KAMPENI ZA DKT. SAMIA ZAPIGA HODI MKOA WA PWANI

BAADA ya kufanya uzinduzi wa kampeni kwenye Uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe ijini Dar es Salaam Agosti 28, 2025, leo Septemba 28, 2025 Mgombea wa Kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan anaingia kwa kishindo mkoa wa Pwani ukiwa ni Mkoa wa 16  baada ya kufanikisha kwa kiwango kikubwa kampeni katika mikoa mingine 15. 


Tanzania Bara ni;  Morogoro, Dodoma, Songwe, Mbeya, Njombe, Iringa, Singida, Tabora, Kigoma, Ruvuma, Lindi na Mtwara.


‎Tanzania Visiwani; Mkoa wa Kusini Unguja, Mkoa wa Kaskazini Unguja, Mkoa wa Kusini Pemba.


Bado mikoa ya; Dar es Salaam,Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara,  Rukwa, Katavi, Shinyanga, Simiyu, Geita, Mara, Kagera, Mwanza, Mkoa wa Mjini Magharibi na Mkoa wa Kaskazini Pemba


‎Akiwa katika mikutano hiyo, Dkt. Samia anajinadi kwa kuelezea mafanikio makubwa ya maendeleo yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita katika  mikoa hiyo, pia hutoa ahadi ya utekelezaji wa miradi mbalimbali.


‎Aidha, Dkt. Samia amekuwa akisisitiza kudumisha Muungano na kuendelea kulinda amani na utulivu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu, ambapo pia amewatoa wananchi wasiwasi kwamba hakutokuwa na vurugu  kwani vyombo vyote vya ulinzi na usalama viko imara, hivyo siku ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29 mwaka huu  wajitokeze kwa wingi tena bila hofu kwenda kupiga kura na kurejea salama majumbani.


‎Pamoja na kuelezea kwa undani Ilani ya uchaguzi ya chama hicho, Dkt. Samia ambaye mgombea wake mwenza ni Dkt. Emmauel Nchimbi, atatumia fursa hiyo kujinadi yeye,  wagombea ubunge na madiwani wa chama hicho.


‎Akiwa katika Mkoa huo Pwani,  atafanya mikutano ya kampeni katika miji ya Kibaha,  Chalinze na Msata, hatimaye kupiga hodi Mkoa wa 16 wa Tanga.



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MBINU ZITAKAZOKUFANYA USIISHIWE PESA

DKT. MIGIRO AKIWASHA KAMPENI ZA DKT. SAMIA MAKAMBAKO

LEO NI LEO KAMPENI ZA DKT. SAMIA SONGWE

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NENO KUNTU LA UMMY MWALIMU ALILOLITOA BAADA YA KUTEMWA KUGOMBEA UBUNGE

CHONGOLO AMKUMBUKA DKT. ASHA-ROSE MIGIRO-