LIJUE CHIMBUKO LA KIMARA

Miaka mingi iliyopita, eneo ambalo leo linaitwa Kimara au Ukanda wa Gaza lilikuwa ni njia ya wasafiri kuelekea maeneo mengine, lakini lilikuwa na misitu mikubwa, wanyama wakali, na hatari nyinginezo za kila aina.
Kulikuwa na mzee mmoja jasiri kutoka Mkoa wa Mara, aliyejulikana kama Mzee Maratu akiishi Maeneo hayo

Km mnavojua watu wa Mara walijulikana tangu zamani kwa ujasiri wao, nguvu za kupambana na mazingira magumu, hawakuwa na hofu ya changamoto. Mzee Maratu pia alikuwa na sifa hizi. 
Alikuwa shupavu, mtu aliyejua jinsi ya kuishi na pori, na alikabiliana na kila hatari kwa busara na nguvu. Alijua namna ya kupambana na wanyama wakali na vibaka waliokuwa wakivizia njiani.

Wasafiri walipopita Maeneo hayo waligundua kuwa Mzee Maratu ndiye aliyewezesha wengi kupita salama katika sehemu hii yenye hatari. Hivyo, walikuwa wakiita eneo hilo kwa shauku:
“Twende kwa yule Mzee wa Mara… kwa Ki-Mara!”

Baada ya muda, jina hili likaanza kubadilika kidogo kidogo, likawa rahisi kutamkwa, na hatimaye likapata jina la Kimara.

Hivyo, jina hili lilibeba alama ya ujasiri, nguvu, moyo usioogopa, na roho ya kujitolea. 
Kimara si jina tu, bali ni kielelezo cha nguvu za kupambana na mazingira magumu, Ushupavu na kujjitolea kusaidia wengine.

Leo hii, unaweza kusikia majina mengi ya Kimara kama vile:
Kimara King'ongo, Kimara Bucha, Kimara Kona, Kimara Baruti, kimara korogwe n.k
#jamiidiary
#makala #article


 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

WALIOCHUKUA FOMU CCM ZA KUWANIA USPIKA HAWA HAPA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HUYU NDIYE WANU HAFIDH, CHAMPIONI WA ELIMU

UKWELI KUHUSU TENDO LA NDOA NA FAIDA ZAKE

MAWAZIRI WALIOACHWA HAWA HAPA

HISTORIA YA MAREHEMU MC PILIPILI