PACOME ASEMA HANA NDOTO ZA KUCHEZA ULAYA

 Staa wa Yanga SC, fundi wa mpira Pacome Zouzou, ametoa kauli ya kushangaza kwa mashabiki wa soka baada ya kusema wazi kupitia tiktok live kuwa hana ndoto ya kucheza Ulaya, akibainisha kuwa kwa sasa anafurahia zaidi maisha yake ndani ya Yanga.


Pacome amesema kuwa lengo lake kubwa si kusaka nafasi barani Ulaya kama ilivyo kwa wachezaji wengi wa Kiafrika, bali anapita katika kipindi kizuri cha maisha na soka lake akiwa Yanga kipindi ambacho hakioni kama anapaswa kukikimbia.


Ameeleza kuwa mazingira ya klabu, mapenzi ya mashabiki, na namna anavyopewa thamani ndani ya timu vinamfanya ajisikie kuwa nyumbani, jambo linalompa nguvu na uhuru wa kucheza kwa kiwango cha juu.


Kauli ya Pacome imeibua mjadala mitandaoni, mashabiki wengine wakimupongeza kwa uaminifu na kujitoa kwake, huku wengine wakiona uwezo wake ungemruhusu kucheza katika ligi kubwa zaidi.


Hata hivyo, Pacome amesisitiza kuwa kwa sasa anajikita kikamilifu katika mafanikio ya Yanga na kutimiza malengo ya klabu ndani ya msimu huu.


๐Ÿ”ฐ

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

UKWELI KUHUSU TENDO LA NDOA NA FAIDA ZAKE

HUYU NDIYE WANU HAFIDH, CHAMPIONI WA ELIMU

MAWAZIRI WALIOACHWA HAWA HAPA

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

๐Œ๐‰๐”๐„ ๐Š๐€๐‚๐‡๐„๐‘๐Ž ๐Œ๐™๐„๐๐€

HISTORIA YA MAREHEMU MC PILIPILI

USIKUBALI KUWA LOFA KWA MWANAMKE...

NAPE AWAPA UKWELI VIJANA