Mwenyekiti wa Taifa, Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC), ametimiza ahadi yake kwa Gereza la Wilaya Korogwe kwa kukabidhi vifaa na fedha taslimu vyenye lengo la kuimarisha ustawi na ujasiriamali leo Wilayani Korogwe, Machi 05, 2026.
Vifaa vilivyokabidhiwa ni pamoja na:
• TV 1 kwa ajili ya gereza.
• Vyerehani 2 vya kisasa.
• Kiasi cha Shilingi Milioni 2 kwa ajili ya Kikundi cha Askari Magereza Wanawake kuanzisha mradi wa Bustani.
Hatua hii ni sehemu ya kuendeleza juhudi za kuwawezesha wanawake kiuchumi na kuboresha mazingira ya kazi na huduma gerezani.
"Uwezeshaji wa Wanawake ni kichocheo cha maendeleo ya jamii nzima."





Comments