Jeshi la Israel limetoa onyo kwa Iran kwamba litaendelea kumsaka kila mrithi wa kiongozi mkuu wa nchi hiyo aliyefariki, Ayatollah Ali Khamenei.
Katika chapisho kwenye X, akaunti ya lugha ya Kiajemi ya IDF ilisema: "Bunge la Wataalamu la Iran, ambalo halijakutana kwa miongo kadhaa, litakusanyika hivi karibuni katika jiji la Qom.
"Tunataka kuwaambia kwamba mkono wa Taifa la Israeli utaendelea kumfuatilia kila mrithi na kila mtu anayetaka kumteua mrithi.
"Tunawaonya wale wote wanaokusudia kushiriki katika mkutano wa uteuzi wa mrithi kwamba hatutasita kuwalenga nyinyi pia. Hili ni onyo!"

Comments