MBUNGE MAJULE KUTOA MSAADA WA VITI BAISKELI 25 KWA WATOTO, WANAWAKE

Mbunge wa Viti Maalumu na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT) Mkoa wa Dodoma, Dkt. Neema Majule katika kuunga mkono tabasamu la Rais Samia Suluhu Hassan kwa Watu wenye ulemavu ameamua kutoa msaada wa viti baiskeli 25 kwa watoto 12 na wanawake 13 mkoani Dodoma. Akizungumza hivi karibuni baada ya kutoa msaada mwingine wa vyakula, vinywaji na vifaa vya usafi kwa Shule ya Viziwi Dodoma, Dkt. Majule ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Rhema Education Foundation aliahidi kutoa msaada huo wa vifaa hivyo saidizi kwa Watu wenye ulemavu, kwa nia ya kupeleka tabasamu, heshima na matumaini mapya kwa Watu wenye ulemavu pamoja na kuwatia moyo na kuimarisha Wanawake wanaolea watoto hao wenye ulemavu. Hafla hiyo ya kukabidhi vifaa hivyo, inatarajiwa kufanyika Machi 8, 2026 majira ya saa 8 mchana katika Kata ya Kiwanja cha Ndege jijini Dodoma.


 IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA - 0754264203

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

Wasifu wa Kizza Besigye

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

IRAN YAMTANGAZA AYATOLLAH MPYA

KILA MWANAMKE ANAPASWA KUFAHAMU HII...

MBUNGE DKT. MAJULE ATOA MSAADA WA VYAKULA, VYANDARUA 100 SHULE YA VIZIWI DODOMA

MAMBO MADOGO YANAYOVUTIA KWA MPENZI WAKO

DKT. MAJULE AKABIDHIWA CHETI CHA SHUKRANI UWT DODOMA KUFANIKISHA USHINDI WA CCM 2025

KWA NINI MAASKOFU JANA KWENYE IBADA YA KUMUAGA PENGO WALIVAA MAVAZI MEUPE WAKATI NI MSIBA..?

WANAOTAZAMWA KUMRITHI AYATOLLAH ALLY KHAMENEI.