SENEGAL YAPINGA VIKALI UAMUZI WA KUNYANG'ANYWA UBINGWA WA AFCON

 Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) limethibitisha kupokea uamuzi uliotolewa na Kamati  ya Rufaa ya CAF kuhusu kupokwa ubingwa wa  Kombe la Mataifa la Afrika 2025 


FSF imepinga rasmi uamuzi huo ambao wanaona hauna msingi wa kisheria, upo kiholela na hauna  uwiano.

FSF inaamini kuna Ukiukaji mkubwa  wa kanuni za  kifungu cha 82 na 84 cha kanuni za CAF zilizohalalisha maamuzi hayo

FSF imeeleza kuwa mwamuzi wa  mechi hiyo alitumia uamuzi wake wa  kuchagua kusimamisha mechi kwa muda na sio kusitisha kabisa. Mchezo ulianza tena, penati ilipigwa, na matokeo ya haki  yalipatikana

Lakini pia wanaamini Utekelezaji wa kifungu cha 84 ni dhuluma. Wachezaji wa Senegal walirejea uwanjani na mwamuzi alithibitisha hilo, mechi ikaendelea hivyo kifungu cha 84 hakiwezi  kufanya kazi

FSF imewaandikia barua CAF ikitaka  wasimamishe  utekelezaji wa uamuzi huu na kusitisha  taratibu zote za kutoa kombe kwa  Morocco ikisubiri usuluhishi wa mwisho lakini pia imeeleza  nia yake ya kwenda kwenye Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo (CAS) ndani ya saa 48 zijazo  ili kutengua uamuzi huu.

Kwenye barua hiyo FSF imeomba kupata ripoti ya waamuzi na maafisa wa mechi hiyo ndani ya masaa 24, isipopata itafungua kesi ya dharula CAS. {Via @officialfelixtz }. 


 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

IRAN YAMTANGAZA AYATOLLAH MPYA

MBUNGE DKT. MAJULE ATOA MSAADA WA VYAKULA, VYANDARUA 100 SHULE YA VIZIWI DODOMA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

Wasifu wa Kizza Besigye

KWA KHERI MAKARANGA UMEUTIMIZA MWENDO...

KWA NINI MAASKOFU JANA KWENYE IBADA YA KUMUAGA PENGO WALIVAA MAVAZI MEUPE WAKATI NI MSIBA..?

WANAOTAZAMWA KUMRITHI AYATOLLAH ALLY KHAMENEI.

MATUKIO RAIS, AMIRI JESHI MKUU DKT. SAMIA AKIZINDUA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA (MMUT)

KIJANA WA KINYAKYUSA WA ENZI HIZO, NUSURA AMCHAPE WAZIRI MUONGO BUNGENI