VIONGOZI WA TACAS WAKUTANA NA SPIKA, MWENYEKITI WA KAMATI BUNGENI

Viongozi wa Chama cha Mawakala wa Forodha (TACAS), wamekutana na kufanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azzan Zungu pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Moshi  Seleman Kakoso bungeni Dodoma mwanzoni mwa wiki.

Wakiongozwa na Mwenyekiti wa TACAS, Ephrahim Rodrick Mwankusye waliwasilisha mbele ya kamati hiyo, baadhi ya kero ambazo walidai  zinasababisha Bandari ya Dar es Salaam kutojiendesha kwa ufanisi, kuelemewa na shehena ya mizigo na foleni ya meli za mizigo. 

Aidha, walitoa ushauri wa jinsi ya kutatua kero hizo kwa lengo la kuboresha uendeshaji wa Bandari hiyo muhimu kwa uchumi wa nchi na tegemeo kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati.

Spika akikabidhiwa zawadi kutoka TACAS.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu,Moshi Selemani Kakoso akiongoza kikao hicho.





 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

IRAN YAMTANGAZA AYATOLLAH MPYA

Wasifu wa Kizza Besigye

MBUNGE DKT. MAJULE ATOA MSAADA WA VYAKULA, VYANDARUA 100 SHULE YA VIZIWI DODOMA

KILA MWANAMKE ANAPASWA KUFAHAMU HII...

KWA KHERI MAKARANGA UMEUTIMIZA MWENDO...

KWA NINI MAASKOFU JANA KWENYE IBADA YA KUMUAGA PENGO WALIVAA MAVAZI MEUPE WAKATI NI MSIBA..?

DKT. MAJULE AKABIDHIWA CHETI CHA SHUKRANI UWT DODOMA KUFANIKISHA USHINDI WA CCM 2025

WANAOTAZAMWA KUMRITHI AYATOLLAH ALLY KHAMENEI.