WMA WATOA ELIMU YA VIPIMO MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Wakala wa Vipimo (WMA) wameshiriki katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Kimataifa, kwa kutoa elimu ya vipimo kwa wadau mbalimbali waliofika Kongwa, Dodoma mahali ambako sikukuu hiyo imefanyika ngazi ya Mkoa.

Akieleza kuhusu huduma zilizotolewa katika maonesho hayo, Meneja Mawasiliano wa WMA, Veronica Simba amesema ni pamoja na elimu kuhusu uandishi wa alama sahihi za vipimo katika bidhaa pamoja na kuhamasisha matumizi ya vipimo sahihi na kwa usahihi.

"Mahala hapa tumekutana na wanawake wengi ambao ni wajasiriamali na tumefanikiwa kuwapatia elimu ya matumizi sahihi ya vipimo kwa ajili ya biashara zao hivyo tumefanikiwa kama tulivyotarajia," amesema.

Vilevile, Simba ameongeza kuwa wamefanikiwa kutoa elimu ya vipimo kwa makundi mengine mbalimbali ya wanawake, wakiwemo watumishi wa umma, wawekezaji na hata kina mama wa nyumbani.

Amesema kuwa, makundi yote hayo yanahitaji elimu kuhusu umuhimu wa matumizi sahihi ya vipimo ili kila mmoja anufaike kulingana na uhitaji wake.










 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

Wasifu wa Kizza Besigye

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

IRAN YAMTANGAZA AYATOLLAH MPYA

KILA MWANAMKE ANAPASWA KUFAHAMU HII...

MBUNGE DKT. MAJULE ATOA MSAADA WA VYAKULA, VYANDARUA 100 SHULE YA VIZIWI DODOMA

MAMBO MADOGO YANAYOVUTIA KWA MPENZI WAKO

DKT. MAJULE AKABIDHIWA CHETI CHA SHUKRANI UWT DODOMA KUFANIKISHA USHINDI WA CCM 2025

KWA NINI MAASKOFU JANA KWENYE IBADA YA KUMUAGA PENGO WALIVAA MAVAZI MEUPE WAKATI NI MSIBA..?

WANAOTAZAMWA KUMRITHI AYATOLLAH ALLY KHAMENEI.