Na Pius Ntiga, Mwaka 2021, Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan alipoahidi ‘kumtua mwanamke ndoo ya maji kichwani,’ maneno yake yaliashiria mabadiliko makubwa katika sera ya maji nchini. Maono hayo sasa yanaanza kutimia, huku serikali ikiwekeza kwa kiasi kikubwa katika upatikanaji wa maji kupitia miradi zaidi ya 100 kote nchini. Kati ya miradi hiyo, hii hapa 25 yenye thamani ya Sh4.15 trilioni ikiwa imebuniwa mahsusi kushughulikia uhaba wa maji kwa kudumu, siyo tu mijini bali hata vijijini, kulingana na takwimu kutoka Wizara ya Maji. Miradi hii inalenga kupunguza mzigo mkubwa ambao wanawake na watoto kwa muda mrefu wameubeba ambapo serikali inalenga kufikia 95% mijini na 85% vijijini ifikapo mwaka 2030. Tukianza na mradi wa Maji Arusha, unaogharimu Sh520 bilioni, unafaidi wakazi 850,000 kwa kuzalisha lita milioni 200 kila siku. Ukikamilika, upatikanaji wa maji mijini utaongezeka hadi asilimia 91.6, huku vijijini wakifikia asilimia 83. Katika mikoa ya Kilimanjaro na Tanga, Mradi wa ...
- Get link
- X
- Other Apps