RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan amesema ameteua aliyekuwa Makamu wa Rais Dk.Philip Mpango kuwa Mshauri wake katika uchumi na miradi na aliyekuwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuwa mshauri wake katika mambo ya jamii. Hivyo amesema kutokana na kuwa na washauri hao katika ofisi yake ndio maana ameamua kufanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri kwa kumteua aliyekuwa Waziri wa Habari,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Profesa Palamagamba Kabudi amemteua kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -Kazi Maalum Akizungumza leo Januari 10,2026 Ikulu Dar es Salaam katika hafla ya kuwapongeza wanamichezo mbalimbali wakiwemo timu ya Taifa Stars iliyofanikiwa kuingia 16 Bora katika michuano ya AFCON ,Rais Samia ametumia nafasi hiyo kuelezea sababu ya kumteua Profesa Kabudi kuwa Ikulu. “Pamoja na kwamba leo ni siku ya kuwapongeza wana michezo waliofanya vizuri kama vijana wangu wa Taifa Stars lakini pia shughuli hii imekuwa wakati maalum kumuaga Profesa Kabudi kuto...
- Get link
- X
- Other Apps