Wataalamu wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Kituo cha King Salman Humanitarian Aid and Relief cha nchini Saudi Arabia wakifanya upasuaji wa kuziba tundu la moyo wa mtoto wakati wa kambi maalumu ya matatibabu inayoendelea JKCI. Watoto 22 wenye matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo wamefanyiwa upasuaji katika kambi hiyo. Na Mwandishi Maalumu - Dar es Salaam. 11/09/2025 Wataalamu wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Kituo cha King Salman Humanitarian Aid and Relief cha nchini Saudi Arabia wamefanya upasuaji wa moyo kwa watoto 22. Upasuaji huo umefanyika katika kambi maalumu ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambapo watoto 40 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa moyo. Akizungumzia jana kuhusu kambi hiyo Mkurugenzi wa Upasuaji wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya alise...
- Get link
- X
- Other Apps