Mwandishi wetu, Morogoro MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima, amewataka Watanzania kuendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani na hata baada ya kumalizika kwa mwezi huo. RC Malima ametoa wito huo wakati akizungumza kwenye futari iliyoandaliwa na Benki ya CRDB kwa ajili ya wateja wake pamoja na wadau mbalimbali wa benki hiyo mkoani Morogoro. Amesema kipindi cha Ramadhani ni muda muhimu kwa waumini wa Kiislamu kujitathmini, kufanya ibada na kuimarisha mahusiano mema, huku akisisitiza kuwa maombi yana mchango mkubwa katika kulinda amani na maendeleo ya taifa. “Niwaombe Watanzania wote kutumia kipindi hiki cha Ramadhani kumuomba Mwenyezi Mungu alinde amani ya nchi yetu na atupe moyo wa upendo na mshikamano ili tuendelee kujenga taifa lenye maendeleo,” alisema Malima. Aidha, alimshukuru Benki ya CRDB kwa kuandaa futari hiyo ambayo imewaleta pamoja viongozi, wateja na wadau mbalimbali katika kuimarisha mahusiano na...
- Get link
- X
- Other Apps