Na Mwandishi wetu,Kibaha Katibu wa Siasa ,Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Dkt. David Mramba amesema ameipongeza kwa dhati hotuba ya Mhe.Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa tarehe Disemba 2 mwaka huu alipozungumza na wazee wa Jiji la Dar es Salaam na kubainisha kuwa imegusa masuala muhimu yanayohusu Taifa na kutoa dira na matumaini makubwa kwa maslahi ya kuleta maendeleo kwa wananchi wa Tanzania. Dkt.Mramba amesema hayo leo tarehe 5 Desemba 2025 katika mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika ofisini kwake Makao Makuu ya CCM wa. Pwani. " Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani kinaunga mkono kwa kauli moja kama ifuatavyo;kuimarisha amani ya Muungano, tunaunga mkono msisitizo wa Mhe. Rais juu ya kulinda amani, utulivu na mshikamano wa Taifa letu kwani amani ndiyo msingi wa maendeleo na hotuba yake imeonesha dhamira ya dhati ya kuendeleza maridhiano,umoja na kudumisha muungano wetu. Mramba amesema kuwa katika kuchoch...
- Get link
- X
- Other Apps