Dunia imejaa makaburi yaliyosheheni hazina kubwa: vitabu ambavyo havikuandikwa, biashara ambazo hazikuanzishwa, na sauti za ukombozi ambazo hazikupazwa. Sababu ya msiba huu wa kimaendeleo si ukosefu wa mtaji wala fursa, bali ni adui mmoja anayeitwa Woga wa Watu. Tumeshikwa mateka na gereza la kisaikolojia lisilo na kuta, ambalo mlinzi wake mkuu ni swali lenye sumu: "Watu watanichukuliaje?" Ukweli mchungu ni kwamba, maisha yako halisi hayajaanza bado; yapo kwenye chumba cha kusubiri (waiting room), yakisubiri saini yako ya ujasiri ili yaanze kuchanua. 1. Gereza la "Watu Watasemaje?" na Upotevu wa Utambulisho Binadamu wengi wanaishi maisha ya "copy and paste" ili tu waonekane wapo sahihi mbele ya macho ya jamii. Tunachagua kozi tusizozipenda, tunao watu wasioendana na maono yetu, na tunafanya kazi zinazofifisha nuru ya roho zetu ili tu kulinda heshima mbele ya watu ambao, kiuhalisia, hawajishughulishi na sisi kiasi hicho. Kama mchambuzi, ni lazima uone ...
- Get link
- X
- Other Apps