. WAHENGA walishasema maisha ni safari ndefu. Ni ukweli ulio dhahiri kwamba viongozi wengi wanaolitumikia taifa hili katika nyadhifa kubwa na tofauti wamepita katika hatua nyingi za maisha tangu kuzaliwa kwao. Miongoni mwa viongozi hao ni Profesa Mark Mwandosya ambaye 2005 alikuwa miongoni mwa makada wa Chama Cha Mapinduzi waliojitokeza kuchukua fomu za kuwania nafasi ya Urais jijini Dodoma. Baada ya hatua hiyo ya kuchukua fomu, Profesa Mwandosya alipaswa kutafuta wadhamini katika mikoa mitano, kabla hajairudisha fomu hiyo kwa ajili ya mchakato wa ndani ya chama. Mchakato huo ulienda safi kwa upande wake alifanikiwa kupata wadhamini na akarudisha Fomu na kuiachia kamati kuu kupendekeza majina matano ambayo yatapelekwa kwenye halmashauri kuu ya CCM. Kikao hicho cha halmashauri kuu, kilipendekeza majina matatu na yeye alitokea kwenye Tatu bora hiyo sambamba na Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Majina matatu alivyopelekwa kwenye mkutano mkuu jina la Dr. Jakaya Kikwete lilupitishwa. Mjue Mwandos...
- Get link
- X
- Other Apps