Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma, Neema Peter Majule, ameishauri Serikali kuboresha utendaji wa Wakala wa usajili, Ufilisi na udhamini (RITA) ili kuondoa ucheleweshaji wa utoaji wa vyeti vya vifo, hali inayowaathiri kwa kiasi kikubwa wananchi hususan yatima na wajane. Akichangia hoja wakati wa uwasilishaji wa bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria Aprili 24, 2026, Bungeni jijini Dodoma, Dkt. Majule amesema RITA ni taasisi nyeti inayogusa moja kwa moja ustawi wa jamii, hivyo kuna haja ya kuongeza ufanisi, kasi na uwajibikaji katika utoaji wa huduma zake. Ameeleza kuwa kuchelewa kupatikana kwa vyeti vya vifo kunakwamisha jitihada za yatima wanaotaka kujiendeleza kielimu pamoja na wajane wanaohitaji kukamilisha taratibu za mirathi, akisisitiza kuwa huduma hizo zinapaswa kutolewa kwa wakati ili kulinda haki za makundi hayo. Katika mchango wake, mbunge huyo pia amepongeza jitihada za Serikali kupitia kampeni ya Mama Samia Legal Aid Campaign, akisema imekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wasi...
- Get link
- X
- Other Apps