Na Victor Masangu,Pwani JUMLA ya miradi 68 yenye thamani ya zaidi ya sh. bilioni 263.1 mkoani Pwani inatarajiwa kupitiwa na mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa katika wilaya saba zenye halmashauri tisa. Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Alhaj Abubakar Kunenge, alisema hayo Aprili 18, 2026 wakati akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka mkoa wa Dar es Salaam katika Shule ya Msingi Mtambani, Mapinga wilayani Bagamoyo. Alisema kati ya miradi hiyo, miradi 23 itawekewa mawe ya msingi, 17 itazinduliwa na 24 itakaguliwa. Baada ya makabidhiano ya kimkoa, Kunenge alimkabidhi Mwenge huo Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Shaibu Ndemanga, ambaye alisema wilaya hiyo ina halmashauri mbili, Bagamoyo na Chalinze ambapo katika Halmashauri ya Bagamoyo, miradi minane yenye thamani ya sh bilioni 11.4 imepitiwa. Katika miradi hiyo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, ameweka jiwe la msingi katika mradi wa kusogeza huduma ya maji safi wa Kibosha–Mapinga unaosimamiwa na DAWASA, utakaogharimu sh...
- Get link
- X
- Other Apps