Benki ya NMB imetoa udhamini wa Sh milioni 100 kwa ajili ya kusaidia maandalizi na uendeshaji wa Mkutano Mkuu wa 40 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) utakaofanyika jijini Arusha. Udhamini huo unaongeza nguvu katika maandalizi ya mkutano huo muhimu unaotarajiwa kuwakutanisha wajumbe kutoka mamlaka mbalimbali za serikali za mitaa nchini. Makabidhiano ya mfano wa hundi hiyo yalifanywa na Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Baraka Ladislaus, kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mkutano huo, Juma Hokororo, katika hafla iliyoshuhudiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa ALAT, Thomas Vungwa. Msaada huo unalenga kuchangia kufanikisha mkutano huo wa uchaguzi pamoja na maandalizi yake kwa ujumla. Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Baraka alisema NMB imeendelea kuwa mshirika wa ALAT kwa zaidi ya miaka 10, jambo linalotokana na kutambua mchango wa jumuiya hiyo katika kusukuma maendeleo kupitia serikali za mitaa. Alisema benki hiyo itaendelea kuunga mkono juhudi zinazosaidia kuimarisha taasi...
- Get link
- X
- Other Apps