Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema Serikali itaendelea kuwaunga mkono wafanyabiashara ndogondogo nchini wakiwemo wasusi, waendesha bodaboda, mama lishe na baba lishe kwa kuwawezesha kupata mikopo yenye masharti nafuu inayotolewa katika halmashauri mbalimbali. Mahundi ameyasema hayo alipohudhuria tamasha la “Urembo na Ibada” lililoandaliwa na mjasiriamali na mmiliki wa saluni, Maria Wilson maarufu kama Chido Point, jijini Dar es Salaam na kukutanisha zaidi ya wanawake 300 Aprili 03, 2026. Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wafanyabiashara ndogondogo ili wajikwamue kiuchumi. “Niwasihi mfike kwenye halmashauri zenu kufuata utaratibu wa mikopo hiyo na kuchangamkia fursa zilizopo. Aidha, nikiwa Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya, nitaendelea kushirikiana na Chido Point katika kuandaa na kuratibu tamasha hili, linalotarajiwa kufanyika mwezi J...
- Get link
- X
- Other Apps