Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeshiriki Mkutano Mkuu maalum wa Chama cha CNDD-FDD cha Burundi uliofanyika Gitega, Burundi leo tarehe 26 Aprili 2026. Ujumbe wa CCM ulioongozwa na Ndg. Suzan Kunambi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) uliwasilisha salamu kutoka kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Mkutano huo ulimchagua Mhe. Evariste Ndaishimiye, Mwenyekiti wa CNDD-FDDd na Rais wa Jamhuri ya Burundi kuwa Mgombea wa Urais katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika nchini Burundi mwaka 2027.
- Get link
- X
- Other Apps