* Mhe. Dkt Akwilapo asisitiza matumizi ya TEHAMA Na Munir Shemweta, WANMM Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amekabidhi jumla ya vifaa vya TEHAMA 1,429 vyenye thamani ya Shilingi Bilioni 5.2 kwa ajili ya Ofisi za Ardhi katika halmashauri 184 nchini, pamoja na ofisi za Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa. Makabidhiano hayo yamefanyika tarehe 23 Januari, 2026, jijini Dodoma, wakati wa kikao kazi kati ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na watumishi wa sekta ya ardhi pamoja na wale wa taasisi zilizo chini ya Wizara. Vifaa vilivyokabidhiwa ni juhudi ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuhakikisha huduma katika sekta ya ardhi zinaimarishwa na kuboreshwa kwa ofisi za ardhi kupatiwa vifaa ili kurahisisha utendaji kazi wao katika kuwahudumia wananchi. Vifaa vya TEHAMA vilivyokabidhiwa ni Kompyuta za kawaida 424, Kompyuta zenye uwezo mkubwa kwa ajili ya kazi za ard...
- Get link
- X
- Other Apps