SEKTA binafsi ambayo ina nafasi ya kimkakati na ya msingi katika utekelezaji wa Dira 2050, ndiyo injini kuu ya ukuaji wa uchumi kupitia uwekezaji, uzalishaji, ubunifu na utoaji ajira nchini. Hayo yameelezwa na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi alipokuwa akifungua Mkutano wa Uhakiki wa Rasimu ya Mpango wa Pili wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (MKUMBI II) kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam Machi 27, 2026. “Mtakumbuka kuwa Mwezi April, 2025, tulizindua Maandalizi ya Mpango wa Pili wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (MKUMBI II) sambamba na Kamati ya Kitaifa ya Wataalamu ya kuandaa Mpango huo.” “Pamoja na mambo mengine, Kamati hiyo ilipewa majukumu ya kuhakikisha MKUMBI II unaandaliwa kwa wakati na kwa kuzingatia ushirikishwaji wa wadau wote katika uwekezaji na biashara ikiwepo sekta binafsi ambayo ina nafasi ya kimkakati na ya msingi katika utekelezaji wa Dira 2050, kwani ndiyo injini kuu ya ukuaji wa u...
- Get link
- X
- Other Apps