SINA budi kuvipongeza vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa kazi kubwa yenye uweledi kwa kudhibiti kwa kiwango cha Juu hali ya usalama wa Nchi Desemba 9, 2025 na kuendelea. Siku hiyo kulikuwa na tishio la uwepo wa maandamano haramu yaliyotangazwa na vibaraka wa mabeberu wasioitakia mema Nchi yetu nzuri Tanzania inayowindwa kila kukicha na mabeberu hao kwa lengo la kupora rasilimali lukuki tulizojaaliwa na Mwenyezi Mungu yakiwemo madini ya thamani kubwa. Mashujaa hao waliofanya kazi hiyo kwa ushirikiano mkubwa ni; Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa, bila kuwasahau wananchi waliotii sheria kwa kukataa kabisa kushiriki maandamano hayo haramu. Pia pongezi za pekee ziliendee Jeshi la Polisi kupitia Msemaji Mkuu wake, David Misime,kwa kitendo cha kutoa mara kwa mara taarifa kwa Wananchi kuhusu hali ya usalama wa Nchi ilivyokuwa inaendelea, hivyo kuwaondolea hofu wananchi. Walienda mbali zaidi kwa kuwaeleza wananchi kuhusu picha za mjonge...
- Get link
- X
- Other Apps