Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ameithibitishia Jumuiya ya Kimataifa kuwa masuala ya demokrasia na haki za binadamu yataendelea kuimarika zaidi nchini Tanzania chini ya uongozi wa Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Balozi Nchimbi aliyasema hayo alipokutana na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Dr. Mehmet Güllüoğlu, Balozi wa Morocco, Mhe. Zacharia El Goumir, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Sera na Tathmini wa Taasisi ya Misaada ya Marekani (MCC), kwa nyakati tofauti, leo Jumanne, tarehe 15 Oktoba 2024. Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, Balozi Nchimbi amesema katika kipindi cha uongozi wa serikali ya awamu ya sita, hatua kubwa imefikiwa katika kuimarisha demokrasia, utawala bora, uchumi na haki za kiraia. Mazungumzo hayo ya Balozi Nchimbi na mabalozi wa nchi hizo, pamoja na taasisi ya MCC, yalilenga kuboresha uhusiano katika nyanja
- Get link
- Other Apps