Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi-CCM, Dokta Asha-Rose Migiro, kesho tarehe 13.1.2026 anatarajiwa kuhitimisha ziara yake ya kimkakati katika wilaya ya Ilala, mkoani Dar es salaam, kwa kuzungumza na Mabalozi wa mashina. Ziara ya Dokta Migiro iliyobeba kauli mbiu isemayo ShinaLakoLinakuita, tayari imeshafanyika katika wilaya ya Temeke, Kigamboni, Ubungo na Kinondoni na kesho itafanyika wilayani Ilala kwa kuzungumza pia na Mabalozi wa mashina katika ukumbi wa Diamond Jublee. Katika ziara yake Katibu Mkuu wa CCM, anazungumzia zaidi nguvu ya wanachama walioko katika mashina, matawi, huku akisisitiza nafasi ya wazee katika kutoa elimu ya itikadi kwa vijana Siku ya kwanza ya ziara, akizungumza na mabalozi wa mashina wa Wilaya za Temeke na Kigamboni katika kikao kazi kilichofanyika ukumbi wa PTA uliopo Sabasaba jijini Dar es Salaam, Dokta Migiro, alisema kuna kila sababu ya kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi kinazingatia utaratibu wa kusikiliza maoni na ushauri kuanzia ngazi ya chini badal...
- Get link
- X
- Other Apps