Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM, DKT. Samia Suluhu Hassan ameahidi kuwalipa fidia wananchi waliopisha ujenzi wa barabara ya Sitalike- Kibaoni mkoani Katavi. Amesema kuwa endapo wananchi watampa ridhaa ya kuongoza tena nchi kwa kumpigia kura katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 29 mwaka huu, ataiagiza Wizara ya ujenzi kufanya upembuzi wa majina ya wanaostahili ili walipwe stahiki zao. Ametoa ahadi hiyo le Oktoba 18, 2025 alipokuwa akijinadi katika mkutano mkubwa wa Kampeni kwenye viwanja vya Azimio Mjini Mpanda mkoani Katavi ikiwa ni siku ya 52 tangubaanze Kampeni Agosti 28, 2025.
- Get link
- X
- Other Apps