Posts
- Get link
- X
- Other Apps
HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI
RAIS TRUMP ARARUANA NA RAIS WA UKRAINE
Rais wa marekani Donald Trump amekutana na Rais wa Ukraine ndugu Volodymyr Zelenskiy pale White House jijini Washington, D.C., February 28, 2025. Mkutano wa Ikulu ya White House kati ya Rais wa Marekani Donald Trump na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy uliolenga kupata makubaliano ambayo yangeruhusu Marekani kupata haki adimu za madini ya Ukrain uligeuka kuwa mechi ya kelele kati ya viongozi hao wawili huku Trump akimtishia Zelenskyy kwa "Utafanya makubaliano au tunatoka." Katika taarifa yake kwenye mitandao ya kijamii kufuatia mkutano huo, Trump alionyesha kuwa makubaliano hayo yamezimwa. "Nimeamua kuwa Rais Zelenskyy hayuko tayari kwa Amani ikiwa Amerika itahusika, kwa sababu anahisi kuhusika kwetu kunampa faida kubwa katika mazungumzo," Trump aliandika. Zelenskiy na Trump wamesuguana kwa hoja na vioja baada ya Zelenskiy kumshutumu Trump kuwa amekuwa laini mno kwa rais wa Russia Vladimir Putin huku Trump akimshutumu zelenskiy kuwa hana...
MWABUKUSI ATOA NENO SIMBA KUSUSIA DERBY DHIDI YA YANGA
Kufuatia kile ambacho kimetokea usiku wa jana kwa klabu ya Simba kuzuiwa kufanya mazoezi ya mwisho katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, na kueleza hawatashiriki mchezo wa Dabi ya dhidi ya Yanga SC. Kupitia mtandao wa X zamani (Twitter) Rais wa Chama cha WanaSheria Tanganyika (TLS) Wakili Boniface Mwabukusi ametoa neno. "Hata kama Simba imezuiwa kucheza ilitakiwa ieleze imechukua hatua gani za kiuongozi kuwasiliana na wahusika baada ya kupuuzwa kwa maelekezo ya Kamishna wa Mchezo. "Huwezi toa tamko kwa umma halafu unaacha maelezo ya msingi na kuishia kusema haki imehifadhiwa ? Ni kukosa umakini je ninyi kama club mumechukua hatua zipi za kusisitiza haki zenu katika kuitaarifu Bodi ya Ligi? au TFF?"
YANGA YATOA TAMKO KALI
MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMAAA....
SERIKALI YALIKUBALI OMBI LA DIAMOND
SERIKALI imesema itajenga Arena yenye uwezo wa kuingiza zaidi ya watu 15,000 katika eneo la Kawe Dar es Salaam. Kauli hiyo inakuja baada ya msanii wa muziki wa kizazi kipya Nassibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kumuomba Rais Samia Suluhu Hassan kuharakisha ujenzi wa Arena ili wasanii wapate ukumbi wa kufanya shughuli zao. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Gerson Msigwa amesema baada ya Rais Samia kufanya ziara Korea, amepata mkopo wa masharti nafuu wa Dola bilioni 2.5. Advertisement “Kati ya fedha hizo ameamua kukata Sh bilioni 450 kwa ajili ya kuzileta Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kujenga Arena kwanza halafu itafuatia kijiji cha filamu,”amesema. Amesema fedha zitakapotoka Korea na kufika kwao wataanza ujenzi wa Arena mara moja ili uwanja huo uanze kutumika kwa ajili ya shughuli za michezo na burudani. “Arena inakuja, ndugu zangu wasanii tumshukuru sana Rais Samia, hili jambo lilikuwa linamu...
HOSPITALI YA MUHIMBILI YAANZISHA HUDUMA YA KISASA YA KUZIBA MAPENGO
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Imeanzisha matibabu ya kuziba mapengo Vipandikizi Meno (Dental Implant), ambapo mzizi bandia hupandikizwa kwenye taya, kisha kuwekewa meno juu yake yanayogandishwa na kutumika kama sehemu ya meno yake ya kuzaliwa nayo. Aidha, Serikali imewezesha hospitali hiyo kununua mashine ya kisasa kabisa inayowezesha uchunguzi wa magonjwa ya mifupa ya taya pamoja na CT scan ya uso na kichwa kusaidia kupanga upandikizaji wa vipandikizi vya meno ambapo tangu kununuliwa mwishoni mwa mwaka 2024 tayari wagonjwa 2,251 wamenufaika. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Huduma ya Upasuaji wa hospitali hiyo, Dkt. Rachel Mhaville alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma Machi 6, 2025, kuhusu mafanikio ya MNH katika miaka minne ya ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan. Dkt. Mhaville ambaye kwenye mkutano huo alikuwa anazungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa M...
ARAJIGA AULA KOMBE LA DUNIA
WAAMUZI wa Tanzania Ahmed Arajiga, Kassim Mpanga, Said Hamdani na Salum Nasir wameteuliwa na na Shirikisho la soka Duniani (FIFA) kuchezesha mchezo wa Kundi G wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2026 kati ya wenyeji Botswana dhidi ya Algeria utakaopigwa Mjini Francistown Nchini Botswana Machi 21, 2025. Algeria na Msumbiji wapo kileleni mwa Kundi G wakiwa na pointi 9 kila mmoja wakifuatiwa na Botswana, Guinea, na Uganda wenye pointi 6 kila mmoja huku Somalia ikiburuza mkia bila pointi yoyote