1. Linda nishati yako. Siyo kila mtu anastahili nafasi katika maisha yako. Wapo wanaoongea sana lakini hawajengi chochote, wanaochosha akili, mioyo, na matumaini. Tambua watu wanaokuchosha na jiondoe. Wema wako haumaanishi ukubali kuumia, kuchoka au kupoteza amani. Linda nguvu yako kama hazina, tumia kwa wanaoithamini. 2. Jifunze kuacha kimya kimya. Siyo kila safari inapaswa kutangazwa, sio kila hatua inahitaji shangwe. Kuna vitu, tabia, na watu wa kuwaachia kimya kimya bila ugomvi, bila maelezo marefu. Ukiona hakikujengi,ondoka. Maisha yanahitaji uamuzi wa ndani, si kelele za nje. 3. Fanya kazi kwenye ndoto zako bila kelele. Mipango yako si ya kila mtu. Wivu, maneno ya kukatisha tamaa, na nguvu mbaya hutokea unapozungumza kabla kutenda. Fanya kazi chini ya maji acha matokeo yaongee. Jenga ndoto zako taratibu, kwa umakini, na kwa bidii. Mafanikio halisi huja kimya lakini sauti yake huisikika mbali. 4. Jipe muda wa kupona. Kupona ni safari, si tukio. Unapopona unajisamehe, unafunga...
- Get link
- X
- Other Apps