UCHAGUZI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa tarehe 29 Oktoba 2025 ulikuwa sehemu ya historia ya maendeleo ya demokrasia ya vyama vingi tangu mwaka 1992. Mamilioni ya Watanzania zaidi ya milioni 31.7 walijitokeza kwa amani kutekeleza haki yao ya kikatiba, ingawa baadhi ya maeneo kama Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya na Songwe yalishuhudia matukio ya uvunjifu wa amani, uporaji, kuchoma moto mali za umma na binafsi kwa kisingizio cha kudai haki. Kuanzia siku ya uchaguzi na siku chache baadae, vurugu zililipuka: vituo vya mafuta vilichomwa moto, magari ya mwendokasi na vituo vyake vikaharibiwa, ofisi za serikali na vituo vya polisi vikaathirika, mali binafsi zikaporwa na kuharibiwa. Jeshi la Polisi na vikosi vya usalama vililazimika kudhibiti hali, maeneo kadhaa yakatiwa ulinzi maalum na mawasiliano ya kidigitali yakadhibitiwa kwa muda mfupi kuzuia taarifa za uchochezi. Uchochezi kutoka mitandao ya kijamii Uchunguzi umebaini kuwa machafuko hayo hayakuwa ya bahati mbaya. Mitanda...
- Get link
- X
- Other Apps