Changamoto za vurugu na maandamano yasiyo na mpangilio huonekana kama njia ya haraka ya kuishinikiza Serikali, lakini kwa Watanzania wengi—hasa wanaothamini amani—mwelekeo huu umeshathibitishwa kuwa ni mkakati dhaifu, usio na uhalali wa kijamii, na usiokidhi misingi ya uzalendo. Ndiyo maana vurugu za #D9 (09 Desemba, 2025) ziligonga mwamba, na ndicho kitakachofanya jaribio lolote la vurugu siku ya Christmas kushindwa vibaya. Sababu zifuatazo zinaeleza kwa kina: 1. *Kukosa Nia Njema ya “Kuandamana”* Maandamano ya kweli huongozwa na hoja halali, dhamira ya haki, na uwazi wa madai. #D9 haikuwa na madai yaliyopimwa—ilikuwa ni wito tu wa vurugu bila suluhisho. Licha ya waandaaji kujinasibu kuwa "Maandamano" hayo ni ya Amani lakini ukiingia kwenye vikao vyao vya ndani walikuwa wakipanga kufanya vurugu za kuchoma majengo muhimu ya serikali, Kuharibu miradi ya kimkakati, kuweka vizuizi kwenye mipaka yetu na hata kuwashambulia wale watakaokaa ndani. Mfano: Katika nchi nyingi za Afrika...
- Get link
- X
- Other Apps