Walokole wengi wanaishi maisha magumu kwa sababu baada ya kuokoka; 1.Walokole wengi baada ya kuokoka wamekosa nafasi ya kufanyiwa maombi ya deliverance. Walokole wengi sana wapo kwenye vifungo kwenye nafsi zao walivyovipata kabla ya kuokoka kutokana na madhabahu za koo zao, uchawi, uganga ,ushirikina waliofanyiwa huko nyuma. Vifungo vya kwenye nafasi haviondoka kwa kuokoka pekee, baada ya kuokoka inabidi ufuate mchakato wa ukombozi. Ukombozi maana yake kurejesha vilivyoibiwa, vilivyoharibiwa au vilivyouwawa na adui ( Yohana 10:10) Mtu anapookoka roho yake ndiyo inayookoka, baada ya kuokoka nafsi yake ndiyo inayotakiwa kushughulikiwa kutoka kwenye vifungo vya ukoo, uchawi, uganga, ushirikina n.k. Walokole wengi sana wanaishi maisha ya vifungo wakidhani ni mapito. Kuna tofauti kati ya mapito na vifungo. Hata kama umeokoka usipotolewa kwenye misingi ya ukoo wenu ambao ulikushikilia hata kabla ya kuokoka kwako utaishi maisha yaleyale wanayoishi ndugu zako ambao hawaj...
- Get link
- X
- Other Apps