Ndugu Wasomaji na Watumiaji wa Blogu Tanzania. Tunapouaga mwaka 2025, nachukua fursa hii, kwa niaba ya wanachama wote wa Tanzania Bloggers Network (TBN), kuwapongeza Watanzania wenzangu kwa kumaliza mwaka huu "kibabe". Tumekuwa na mwaka wenye matukio mengi ya kihistoria, na ninyi wasomaji wetu mmekuwa wadau muhimu kwa kufuatilia habari, uchambuzi, na taarifa mbalimbali kupitia majukwaa yetu ya kidijitali. Kuelekea Mwaka 2026: Makubwa Zaidi Yanakuja! Mwaka 2026 unakwenda kuwa mwaka wa mageuzi makubwa kwa TBN. Tunatarajia kuleta maudhui yenye ubunifu wa hali ya juu, habari za kina, na teknolojia ya kisasa zaidi katika kuhabarisha umma. Wanachama wetu wamejipanga kuwa daraja imara zaidi kati ya serikali na wananchi, tukihakikisha kila Mtanzania anapata habari sahihi na kwa wakati. Ombi Langu kwa Watanzania: Tunapoingia 2026, rai yangu ni kuendelea kudumisha amani na utulivu. Tuepuke vurugu na migawanyiko, badala yake tujikite katika umoja wetu kama Taifa. Huu ni wakati wa kuung...
- Get link
- X
- Other Apps