Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Emmanuel Nchimbi akikaribishwa rasmi nyumbani kwao Mkoa wa Ruvuma kwa kufanyiwa kimila na machifu pamoja na wazee wa jadi alipofika eneo la Mnara wa Kumbukumbu ya Mashujaa wa Vita vya Maji Maji mjini Songea Aprili 20, 2024. Katika ziara hiyo, Dkt. Nchimbi ameambatana na wajumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla pamoja na Katibu wa Oganaizesheni, Issa Haji Gavu. Kiongozi huyo mtendaji mkuu wa CCM, atakuwa mkoani Ruvuma ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya siku 10 katika mikoa ya Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Ruvuma. Lengo la ziara hiyo ni kuimarisha uhai wa chama, kutatua kero za wananchi, kuelezea maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu na Uchaguzi Mkuu mwakani, kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya chama hicho. Baada ya kumaliza katika mikoa ya Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya na Njombe, ziara hiyo ya siku 10 yenye mafaniki
Comments