Makundi maalumu 27,946 yamesajiliwa kwenye m fumo wa NeST na ku pata zabuni zenye jumla ya thamani ya Shilingi Bilioni 56 , kupitia Mfumo huo. makundi ya vijana ni 13, 317 wanawake 13,400 , wazee 643 na watu wenye ulemavu 586. Hayo yemebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Dennis Simba wakati wa mkutano na vyombo vya habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO, katika Mji wa Serikali wa Mtumba jijini Dodoma, Agosti 20, 2026. Sheria ya Ununuzi wa Umma, imezielekeza taasisi zote za umma kutenga asilimia 30 ya bajeti zao za ununuzi kwa ajili ya makundi maalum (vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu). Lengo la PPRA, kwa kuzingatia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ni kuwa na takribani makundi 300,000 yaliyo tayari kuomba zabuni. Hatua hii ni sehemu ya jitihada za Serikali kutoa ajira na kazi kwa Watanzania ambao hawana uwezo wa kuwa na kampuni, ambao wanaweza kujiunga k...
Comments