DKT. NCHIMBI AWAPOKEA VIONGOZI WA CHADEMA, ACT WALIOHAMIA CCM

.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akizungumza na umati mkubwa wa wananchi Namtumbo, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Namtumbo, leo Alhamis tarehe 3 Aprili 2025. 

Katika mkutano huo, viongozi wa vyama vya ACT Wazalendo na Chadema, wakiwaongoza wanachama wao, waliamua kurejesha kadi na vifaa vingine vya vyama hivyo, kisha wakajiunga CCM.

Viongozi hao, akiwemo Ndugu Alifa Jafa, Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Songea, Ndugu Mohamed Said Ndauka, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Ntungwe na Azarius Lucas Ngonyani, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Miembeni, walieleza jinsi ambavyo uongozi wa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na kuteuliwa kwa Balozi Nchimbi kuwa mgombea mwenza wa Urais, kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 2025, umewavutia kuhamia CCM.








 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MWANAMKE ALIYEVUNJA REKODI KWA KUZAA WATOTO 69

BODI YA LIGI YAKIRI MAKOSA, WAIOMBA YANGA WAYAMALIZE

#MAKINIKIA: HEKAYA FUPI YA MJI WA KIHISTORIA WA MOSHI MKOANI KILIMANJARO

HUU NDIO UKWELI ULIVYO RAFIKI YANGU

BODI YA LIGI SASA WAOMBA HEKIMA NA BUSARA ITUMIKE DERBY YA YANGA, SIMBA

RATIBA KAMILI YA HARUSI YA DIAMOND, ZUCHU

ZIJUE TABIA 9 ZA WANAWAKE HAWA....

TANZANIA NI MIONGONI MWA NCHI 10 ZINAZOONGOZA KWA MAZAO YA KILIMO AFRIKA