TIMU ya Simba imefanikiiwa kwenda Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya sare ya bila kufungana na wenyeji, Stellenbosch katika mchezo wa marudiano wa Nusu Fainali jioni ya leo Uwanja wa Moses Mabhida Jijini Durban, Afrika Kusini
Simba wananufaika na ushindi wa 1-0 kwenye mchezo wa kwanza wa Jumapili iliyopita Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar, bao pekee la kiungo wa Muivory Coast, Jean Charles Ahoua dakika ya 45'+2.
Simba sasa inasubiri mshindi wa jumla kati ya RSB Berkane ya Morocco na CS Constantine ya Algeria ambazo zinarudiana leo kuanzia Saa 1:00 usiku Uwanja wa Mohamed-Hamlaoui Jijini Constantine.

Comments