TBC KUFANYIWA MABORESHO MAKUBWA

 


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Paramagamba Kabudi amesema lengo la kuanzisha Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari ni kuifanya Taaluma ya uandishi wa habari iheshimike sawa na taaluma za uhandisi, udaktari na uanasheria.


Aidha, amesema kuwa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), litafanyiwa maboresho makubwa ikiwemo usikivu na kuanzishwa wa idha ya nje kwa lugha ya kiingereza.

Pamoja na mambo mengine Prof. Kabudi ameyasema hayo katika Ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma Aprili 14, 2025, alipofungua dimba la mawaziri kuzungumza na vyombo vya habari kuhusu kuhusu mafanikio ya wizara katika kipindi cha uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamadunim Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa akitoa neno la utangulizi alipokuwa akimkaribisha Waziri Kabudi.

Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.
Waziri Kabudi akiwa na wanahabari.

Msigwa akiwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari MAELEZO, Rodney Thadeus.
 IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
MSIMAMIZI MKUU
KAMANDA WA MATUKIO ONLINE TV
0754264203

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

BREAKING NEWS | MKURUGENZI MTENDAJI WA TANESCO AFARIKI DUNIA

BODI YA LIGI YAKIRI MAKOSA, WAIOMBA YANGA WAYAMALIZE

#MAKINIKIA: HEKAYA FUPI YA MJI WA KIHISTORIA WA MOSHI MKOANI KILIMANJARO

HUU NDIO UKWELI ULIVYO RAFIKI YANGU

RATIBA KAMILI YA HARUSI YA DIAMOND, ZUCHU

ZIJUE TABIA 9 ZA WANAWAKE HAWA....

TANZANIA NI MIONGONI MWA NCHI 10 ZINAZOONGOZA KWA MAZAO YA KILIMO AFRIKA

YANGA YACHINJA NG'OMBE 20 ZA PILAU TABORA