Vitabu vipya viwili vya rangi vya Jimbo la Musoma Vijijini vinavyoelezea Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020-2025 vinachapishwa na vitaanza kugawiwa bure kuanzia tarehe 30.5.2025
Vitabu hivyo ni:
*Volume VI (Mwaka wa Fedha 2023/2024), 102pp
*Volume V (Mwaka wa Fedha 2022/2023), 86pp
Kitabu cha Mwaka wa Fedha 2024/2025 (Volume VII) kitachapishwa baada ya tarehe 30.6.2025
Vitabu vingine vya Jimbo hili ambavyo vimechapishwa na kugawiwa bure ni: Volumes I, II, III na IV.
Vitabu vyote hivi vinaelezea miradi inayobuniwa na kuanza kutekelezwa na wanavijiji na Mbunge wao, na baadae Serikali huchangia ukamilishaji wa miradi ambayo ni ya wanavijiji.
Orodha ya wachangiaji wa kila mradi imetolewa, na imetunzwa na kila serikali ya kijiji yenye mradi unaotekelezwa
Vilevile, miradi inayotekelezwa kwa asilimia 100 (100%) na Serikali nayo imeelezwa.
Tovuti ya Jimbo:
Vitabu vyote hivyo na taarifa nyingine muhimu za maendeleo na ustawi wa Jimbo la Musoma Vijijini vinapatikana kwenye Tovuti hiyo ambayo ni:
www.musomavijijini.or.tz
Picha iliyoambatanishwa hapa inaonesha:
Vitabu 2 vipya vya Utekelezaji wa Ilani ya CCM ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini vitakavyoanza kugawiwa bure tarehe 30.5.2025
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz
P. O. Box 6
Musoma
Tarehe:
Jumapili, 18 May 2025

Comments