WAZIRI MAVUNDE AONGOZA WATUMISHI KUHAMIA JENGO LAO JIPYA MTUMBA

 

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, ameongoza watumishi wa wizara hiyo leo Mei 15, 2025 kuanza rasmi kazi katika jengo jipya la kisasa lililopo eneo la Mtumba, jijini Dodoma.

Uhamisho huo unamaanisha kuwa huduma zote za Wizara sasa zitapatikana katika eneo moja, hatua inayolenga kuondoa usumbufu uliokuwa ukiwakumba wananchi waliolazimika kufuata huduma katika maeneo tofauti .

Akizungumza Mei 15,2025 kwenye Ofisi za Wizara hiyo wakati wa kuwasili kwa mara ya kwanza katika jengo hilo, Waziri Mavunde amesema kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo la Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini lililotaka wizara hiyo kuhamia katika Ofisi hiyo .

Ameongeza kuwa amekamilisha ahadi yake ya kuhakikisha wizara hiyo inahamia rasmi kama sehemu ya mageuzi ya kiutendaji.

Waziri huyo ameeleza kuwa kukamilika kwa jengo hilo ni matokeo ya usimamizi mzuri na mshikamano wa watumishi wa wizara na kuwapongeza kwa kazi kubwa waliyoifanya kuhakikisha mradi huo wa unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa.

Amesema kuwa hatua hiyo ni ushahidi wa namna Serikali ilivyojipanga kuboresha huduma kwa wananchi.

“Tunataka wananchi wapate huduma kwa urahisi bila kukimbizana kutoka ofisi moja hadi nyingine,kwa sasa, vitengo vyote muhimu vya wizara vinapatikana hapa Mtumba,hii ni hatua kubwa ya kuimarisha utendaji wetu,” amesema Mavunde.

Mbali na kuwahakikishia wananchi huduma bora, Waziri Mavunde ameeleza kuwa wafanyabiashara waliopo katika sekta ya madini nao watanufaika na uboreshaji wa miundombinu hiyo.

Amesema mazingira bora ya kazi yanayopatikana Mtumba yataongeza ufanisi katika utoaji wa leseni, usimamizi wa shughuli za uchimbaji na ufuatiliaji wa sekta kwa ujumla.

Waziri Mavunde amewataka watumishi wote wa Wizara ya Madini kuendelea kuwa weledi na wawajibikaji katika kuhudumia wananchi, akisema kuwa jengo jipya ni fursa mpya ya kuonyesha mabadiliko katika utoaji wa huduma bora kwa taifa.












Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

UKWELI KUHUSU TENDO LA NDOA NA FAIDA ZAKE

HUYU NDIYE WANU HAFIDH, CHAMPIONI WA ELIMU

MAWAZIRI WALIOACHWA HAWA HAPA

๐Œ๐‰๐”๐„ ๐Š๐€๐‚๐‡๐„๐‘๐Ž ๐Œ๐™๐„๐๐€

HISTORIA YA MAREHEMU MC PILIPILI

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

USIKUBALI KUWA LOFA KWA MWANAMKE...

NAPE AWAPA UKWELI VIJANA