CHINA NI TAIFA LA WATU IMARA, WENYE HESHIMA

China ni Taifa lenye watu Imara sana na wenye heshima Popote wawapo Dunaini, Kuna watu Wameniuliza Inakuaje Washirika wa China, ukitokea mgogoro wa ndani katika Nchi yoyote mshirika wa China hua china inaondoka katika Eneo hilo bila kutoa msaada wa kijeshi? 

Mfano: Sudan Darfur ni mshirika Mkubwa wa China ila Baada ya migogoro ya wao kwa wao, China Imeondoka Nchini Sudan kiasi kwamba Wengine wanachukulia kua China ni Dhaifu.

Kwakua mimi Chotara Mweusi Sultan ndio Profesa wa Uchambuzi wacha Niwapeni Elimu kuhusu hilo Muelewe China Na sera zake za Mambo ya Nje.

Sera ya China ya kutoingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine Yani non-interference ina mizizi ya kihistoria, kimkakati na kiitikadi.

China ilipitia karne ya fedheha ๐Ÿ‘‰Century of Humiliation kuanzia karne ya 19 hadi katikati ya karne ya 20, ilipovamiwa, kugawanywa na kudhibitiwa na mataifa ya Magharibi na Japani.

China ilijifunza kuwa kuingiliwa kwa mambo ya ndani ni chanzo cha kudhoofisha taifa. Ndiyo maana๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Inapinga vikali uingiliaji wa nje
๐Ÿ‘‰Inaheshimu mamlaka kamili ya taifa

Tangu 1954, sera ya nje ya China imejengwa juu ya kanuni Kuu tano๐Ÿ‘‡
1๐Ÿ‘‰Kuheshimiana kwa mamlaka ya kitaifa
2๐Ÿ‘‰ Kutokuingilia mambo ya ndani
3๐Ÿ‘‰Kutokushambuliana
4๐Ÿ‘‰Usawa na manufaa ya pande zote
5๐Ÿ‘‰Kuishi kwa amani

 Kanuni hizi ndizo msingi wa mahusiano yake na Afrika, Asia na Amerika ya Kusini. Maslahi ya kiuchumi, Biashara bila masharti ya kisiasa

China inaamini kuwa ๐Ÿ‘‰Kila taifa lina njia yake ya maendeleo
๐Ÿ‘‰Demokrasia au mfumo wowote wa utawala si sharti la biashara

Tofauti na Marekani au Ulaya ๐Ÿ‘‰huambatanisha biashara na masharti ya kisiasa kwa Mgongo wa demokrasia na haki za binadamu

China Inatoa mikopo na uwekezaji bila masharti ya Kuingilia mambo ya ndani ya Nchi yoyote Yani Kama mtagombana Nyie kwa nyie sio jukumu la China kuingilia upande wowote katika mgogoro wenu wa ndani Zaidi mjitafakari na mjenge Nchi Yenu.

Sera kama Hii ya China huwafanya washirika wake wengi wajisikie huru na kuheshimiwa

China inahitaji sana Kuepuka kurudia kile ilichokipinga, China huona uingiliaji wa kijeshi au kisiasa kama๐Ÿ‘‡

๐Ÿ‘‰Ubeberu mpya Waingereza wanaita neo-colonialism
๐Ÿ‘‰Njia ya mataifa makubwa kudhibiti rasilimali za wengine

Hivyo basi๐Ÿ‘‰  “Hatufanyi kwa wengine kile tulichofanyiwa.” sera ya China.

China hujenga Mkakati wa muda mrefu wa ushawishi wa kimya China haingilii Sera ya mambo ya ndani ya Nchi yoyote, lakini

๐Ÿ‘‰Huongeza uwepo wa kiuchumi
๐Ÿ‘‰Huunda utegemezi wa kibiashara
๐Ÿ‘‰Hujijengea ushawishi wa muda mrefu bila vita

Ushawishi huu ni wa kiuchumi, si wa kijeshi wala kisiasa moja kwa moja. Sababu ya ndani ya China yenyewe China ina
๐Ÿ‘‰Xinjiang
๐Ÿ‘‰Tibet
๐Ÿ‘‰Hong Kong
๐Ÿ‘‰Taiwan

Ikiwa ingeruhusu kuingilia Sera ya mambo ya ndani ya mataifa mengine, Ingehalalisha mataifa hayo kuingilia masuala yake ya ndani

๐Ÿ‘‰Kwa hiyo inalinda sera hii kwa maslahi yake binafsi. Unajisikiaje Jirani yako anakuja kuingilia Ugomvi wako wewe na mkeo Alafu anakaa upande mmoja? Yani anampa nguvu mkeo alafu wewe anakubeza ? China haipendi hivo inaamini Kwamba Waathirika si majirani bali ni ninyi wenyewe.

Huu ndio Mtazamo wa China juu ya migogoro ya ndani China huamini๐Ÿ‘‡

๐Ÿ‘‰Migogoro ya ndani lazima itatuliwe na wenyewe
๐Ÿ‘‰Mazungumzo ya ndani ni bora kuliko shinikizo la nje

Ndiyo maana mara nyingin Hupiga kura ya kujizuia kwenye Baraza la Usalama la UN, Hupendelea diplomasia tulivu badala ya adhabu au vikwazo

Baki na Mimi kwa Mengi zaidi yanayo jiri Duniani 

By Professor Chotara Mweusi Sultan kutoka viunga vya ๐Ÿ‘‡ 
๐Ÿ‘‰Sharif shamba 
๐Ÿ‘‰Ilala Dar es salaam 
๐Ÿ‘‰Tanzania 

Bingwa la uchambuzi wa maswala ya kijamii, Uchumi na Siasa za Dunia Yetu.



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

UKWELI KUHUSU TENDO LA NDOA NA FAIDA ZAKE

HUYU NDIYE WANU HAFIDH, CHAMPIONI WA ELIMU

MAWAZIRI WALIOACHWA HAWA HAPA

๐Œ๐‰๐”๐„ ๐Š๐€๐‚๐‡๐„๐‘๐Ž ๐Œ๐™๐„๐๐€

HISTORIA YA MAREHEMU MC PILIPILI

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

USIKUBALI KUWA LOFA KWA MWANAMKE...

NAPE AWAPA UKWELI VIJANA