"WHO ARE YOU" ONYO LILILOZAA MATUNDA KIUCHUMI

Kwanza Inatupasa Kufahamu zama zimebadilika mikakati ya Kuwakataa Wanyonyaji Inaendelea Afrika nzima kwasasa Tahadhari ni kubwa sana kwa Nchi za Magharibi Husasa Nchi kama ya Umoja wa majimbo (Marekani)

Marekani hupendelea kufanya kazi na mataifa Imara yani ๐Ÿ‘‰stable nations

Fahamu kua Sera ya nje ya Marekani inatoa kipaumbele kwa๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Utulivu wa kisiasa
๐Ÿ‘‰Utabiri wa sera Yani policy predictability
๐Ÿ‘‰Mazingira rafiki kwa uwekezaji
๐Ÿ‘‰Utawala wa sheria na uhuru wa kiuchumi

Kama Mnavyo Fahamu Tanzania imekuwa Muhimili wa utulivu katika Ukanda wa Afrika Mashariki kwa miongo Na Miongo. Hili linaiweka Tanzania kwenye kundi la nchi ambazo Marekani na nchi za Magharibi hutaka kulinda mahusiano nao kuliko kuyavuruga.

Inatakiwa Tufahamu Kwa nini Marekani haiwezi kuruhusu uhusiano na Tanzania kuharibika, Tanzania ina umuhimu wa kimkakati yani strategic importance kwa sababu๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Ni kitovu cha kijiografia Afrika Mashariki.
๐Ÿ‘‰Ina rasilimali muhimu kama gesi, madini. muhimu kwa teknolojia, nishati.
๐Ÿ‘‰Ni lango la kibiashara kwa SADC na EAC.
๐Ÿ‘‰Ina bandari muhimu ya Dar es Salaam na Bagamoyo.
๐Ÿ‘‰Ni nchi yenye utulivu wa kijamii na kisiasa.
๐Ÿ‘‰Ni Nchi isio Yumbishwa Katika sera zake za mambo ya ndani. 

Kwa Marekani, kupoteza ushawishi Tanzania kungekuwa na madhara makubwa sana kama๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Kupoteza Mshirika muhimu 
๐Ÿ‘‰Kuipa Nafasi Zaidi China na Urusi.
๐Ÿ‘‰Kuporomoka kwa ushawishi wa Magharibi Afrika Mashariki, hususa wakati China na Urusi wanaimarisha uwepo wao Kwa Kasi na nguvu nyingi.

Ziara ya Kaimu Balozi wa Marekani Ikulu na Mazungumzo Na Mh Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuhusu  “mabilioni” Hii inaonyesha mambo mawili makubwa
๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Marekani imepokea ujumbe wa Tanzania wa kutaka usawa (win–win)

Hotuba ya Rais iliyo na kauli kama “Who are you?” iliwafikisha moja kwa moja Wamagharibi kwamba
๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Tanzania haitakubali tena mikataba ya kinyonyaji.
๐Ÿ‘‰Hakutakuwa na ubabe wa kiuchumi.
๐Ÿ‘‰Ushirikiano lazima uwe wa maslahi ya pande zote.

Badala ya kukasirika kwa Kauli hiyo, Marekani imechukulia kauli hiyo kama.
๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Ukweli wa kisera, sio matusi.
๐Ÿ‘‰Onyo la kidiplomasia kwamba zama za "take it or leave it" zimepitwa na wakati.
๐Ÿ‘‰Ishara ya kwamba Tanzania sasa inajiamini kimataifa.

Marekani haitaki kupoteza nafasi zake kwa China au Urusi Kitu ambacho Marekani imewahi Mapema kujisalimisha Yani Kuingia Ikulu kwa mazungumzo ya kiwango cha mabilioni kunaonesha kwamba
๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Wanaokoa nafasi zao kabla haijachukuliwa na mataifa mengine.
๐Ÿ‘‰Wanaonesha kuwa bado wapo tayari kushindana kwa ustaarabu.

Athari ya Uwepo wa Urusi Tanzania Hili ndio sehemu muhimu zaidi ya geostrategy Uwepo wa Urusi (uwekezaji, mafunzo, nishati, usalama) unasababisha
๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Marekani na Magharibi kuongeza uwazi katika mikataba.
๐Ÿ‘‰Kupungua kwa masharti ya kibeberu
๐Ÿ‘‰Ushindani wa kimaendeleo ambao Tanzania inanufaika nao
๐Ÿ‘‰Majadiliano kuwa ya heshima zaidi, si ya kulazimisha

Kwa maneno mengine Tunasema kwamba
๐Ÿ‘‰Tanzania imeongeza "bargaining power".

Tanzania kama Taifa la Kimkakati Ukanda wa Afrika mashariki na Nchi za Maziwa makuu Bila kusema kubwabwaja ukweli ni huu
๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Tanzania sasa haipigiwi debe kama nchi dhaifu ya kutegemea misaada.
๐Ÿ‘‰Ni mchezaji muhimu katika usalama wa Afrika Mashariki, madini muhimu (helium, graphite, nickel), na njia za biashara.

Tazama Dunia inavyogawanyika upya yani East vs West, Tanzania imeendelea chukua msimamo wa non-alignment ya kisasa zaidi.
๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Inafanya kazi na Marekani
๐Ÿ‘‰Inaendelea na China
๐Ÿ‘‰Inafanya kazi na Urusi
๐Ÿ‘‰Inashirikiana na Mataifa ya Ghuba Uwajemi na Asia

Hii ni diplomasia ya "Rarafiki wa wote, Asie na Adui" Sera ambayo mataifa mengi makubwa wanaiheshimu. ๐Ÿ‘‰"Win–Win Situation” ndiyo msingi wa uwezo wa Tanzania kwasasa Atakae na aje.

Tanzania Ya sasa haiendi Washington au Moscow kama Omba Omba bali kama
๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Nchi yenye rasilimali
๐Ÿ‘‰Soko la watu milioni 70+
๐Ÿ‘‰Kituo cha utulivu
๐Ÿ‘‰Mlango wa uchumi wa kikanda
๐Ÿ‘‰Nchi inayojitegemea kimkakati

Kwa hiyo Magharibi wanakuja kwa msimamo wa๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Kusikiliza
๐Ÿ‘‰Kutiwa hofu kidogo
๐Ÿ‘‰Kutaka kulinda maslahi yao bila kupoteza ushawishi

Ifahamike kwamba baada ya Nchi Nyingi za Magharibi Kupoteza Ushawishi wao Ukanda wa Sahel na Kusini mwa Afrika Kumeifanya Tanzania ikae kwenye kipindi cha historia ambacho๐Ÿ‘‡
๐Ÿ‘‰Ushawishi wake unaongezeka kimataifa.
๐Ÿ‘‰Mamlaka yake ya majadiliano imeimarika.
๐Ÿ‘‰Mataifa makubwa yanashindana kwa heshima kutaka ushirikiano na Tanzania.

Kauli za uthubutu kutoka kwa viongozi, ikiwemo “Who are you?”, zimewafanya Magharibi kutambua kuwa zama zimebadilika Sio kila Homa ni Malaria zinge Ni kaswende.

Huu ndio msingi wa kuwa taifa la kimkakati, na Tanzania kwa sasa iko hapo katikati ya nguvu mbili kubwa duniani Yani West na East, ikicheza mchezo wake kwa ustadi.

Nimalize kwa kusema Mwenyezi Mungu Ibariki Tanzania wabariki Viongozi wetu na Utubariki watanzania wote.

Baki na Mimi kwa Mengi zaidi yanayo jiri Duniani 

By Professor Chotara Mweusi Sultan kutoka viunga vya ๐Ÿ‘‡ 
๐Ÿ‘‰Sharif shamba 
๐Ÿ‘‰Ilala Dar es salaam 
๐Ÿ‘‰Tanzania 

Bingwa la uchambuzi wa maswala ya kijamii, Uchumi na Siasa za Dunia Yetu.



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

UKWELI KUHUSU TENDO LA NDOA NA FAIDA ZAKE

HUYU NDIYE WANU HAFIDH, CHAMPIONI WA ELIMU

MAWAZIRI WALIOACHWA HAWA HAPA

๐Œ๐‰๐”๐„ ๐Š๐€๐‚๐‡๐„๐‘๐Ž ๐Œ๐™๐„๐๐€

HISTORIA YA MAREHEMU MC PILIPILI

USIKUBALI KUWA LOFA KWA MWANAMKE...